Serikali ya Morocco yakubaliana haya na Tanzania

In Uchumi

Serikali ya Morocco imesema kuwa iko tayari kushirikiana na Tanzania katika suala zima la kukabiliana na athari zitokanano na mabadiliko ya tabianchi kwa kuwekeza kati mradi mkubwa wa Nishati ya jua.

Hayo yamesemwa na Balozi wa Morocco hapa nchini, Benryane Abdelilah Jijini Dar es salaam alipokuwa akizungumza na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina amesema kuwa Morocco ipo tayari kuwekeza katika mradi mkubwa wa Nishati ya Jua ‘Solar energy’, ili kuweza kusaidiana na Tanzania katika suala zima la kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.

Amesema kuwa Idara ya Mazingira inatakiwa kuainisha maeneo ya vipaumbele kwa upande wa mazingira na kusema  kuwa, mradi huo mkubwa wa uzalishaji wa  Nishati ya jua utakaotekelezwa na kampuni kutoka Morocco ya Masen Campany Limited,

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina amesema kuwa kabla ya uwekezaji wa mradi mkubwa wa aina hiyo, inatakiwa ifanyike tathmini ya athari ya mazingira na kuahidi kuwa watakapokuwa tayari zoezi hilo litafanyika kwa haraka.

Hata hivyo, Balozi Benryane Abdelilah amesema kuwa utatuzi wa tatizo hilo la mabadiliko ya tabianchi utasaidia kuokoa kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira hapa nchini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu