Serikali kupitia wa naibu waziri wake wa mali asili na utalii
ndugu Constantine Kanyasu,imesema kuwa imeondoa tozo ya
dola 1500 kwa wawekezaji wa ndani pamoja na masharti ya
idadi ya usajili wa magari kwenye uwekezaji.
Mheshimiwa Kanyasu amesema wamefanya hivyi ili kuwezesha
kampuni za wazawa wanaowekeza kwenye utalii,kuwekeza kwa
wingi kwenye hifadhi za wanyama ili kuchochea na kukuza
utalii wa Tanzania.