Serikali za Uingereza na Marekani, zatoa msaada wa Euro milioni 40.4 sawa na (Sh bilioni 101) kwa Serikali ya awamu ya tano.

In Kitaifa

Jumuiya ya kimataifa imeendelea kuiunga mkono Serikali ya Awamu ya Tano katika hatua zake za kuwaletea wananchi maendeleo, ambapo Umoja wa Ulaya (EU), Serikali za Uingereza na Marekani, kwa pamoja, zimetoa msaada wa Euro milioni 40.4 sawa na  (Sh bilioni 101).

Fedha hizo ni kwa ajili ya kufadhili ujenzi wa barabara kuanzia Kidatu-Ifakara mkoani Morogoro, itakayojengwa kwa kiwango cha lami.

Kupatikana kwa fedha hizo, mbele ya uwakilishi wa EU, Wizara ya Fedha na Mipango imetiliana saini na Kampuni ya ujenzi wa barabara ya Reynolds, kandarasi ya ujenzi wa barabara hiyo, yenye urefu wa kilometa 67.

Mkataba huo umesainiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Amina Shaaban, kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Dan Yzhak Shahn, ambaye ni Mkandarasi kutoka Kampuni ya Ujenzi ya Reynolds.

Kiasi hicho cha fedha ni sawa na Euro milioni 40.4 ambapo Euro milioni 29.6 zimetolewa kwa ushirikiano wa Umoja wa Ulaya na Shirika la Misaada la Uingereza (UKAID), huku kiasi kinachobaki cha Euro milioni 10.8 kikitolewa na Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID).

Akizungumza  mara baada ya kutiwa saini kwa kandarasi hiyo, Naibu Katibu Mkuu amesema ujenzi wa barabara hiyo utakaohusisha pia ujenzi wa daraja la Mto Ruaha Mkuu, utasaidia wakulima wadogo kupitia Programu ya Uendelezaji Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), walioko katika Bonde la Mto Kilombero, kuyafikia masoko ya uhakika ya mazao yao.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu