Shule ya mchepuo wa kiingereza ya Ngorika Happy Watoto iliyopo kata ya Maji ya Chai Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha leo imefanya ziara katika kituo cha habari na matangazo cha TAN COMMUNICATION MEDIA RADIO 5 kilichopo Njiro Jijini Arusha.
Akizungumza ndani ya kituo hicho Mwalimu wa somo la sayansi aliyeongozana na Wanafunzi hao Mwl.Ruben Magawa amesema lengo la ziara hiyo ni kujifunza technolojia mbalimbali zinazohusiana na habari ikiwa ni pamoja na Wanafunzi wake kujifunza somo la mawasiliano.
“Mazingira yako kimya, nimeona chumba kipo kimya sanaa nimeona wataangazaji mubashara kwa mara ya kwanza na tumejifunza umuhimu wa radio kwa kusambaza elimu kutoa taarifa kwa watu wengi” amesema mwalimu Ruben
Hata hivyo amewataka Wadau wa elimu waige mfano kwa kufanya ziara ya kutembelea vyombo vya habari kwa kujifunza mambo mbalimbali na anatarajia watoto wake wafike mbali.