Simba yawatambia Mwadui

In Michezo

Afisa habari wa Simba Haji Manara amesema kuelekea mchezo wa Ligi kuu soka Tanzania bara leo Juni 20, 2020, kati ya Simba dhidi ya Mwadui FC, hawatarajii kama kutakuwa na matokeo matatu.

Kupitia taarifa aliyotuma kwa vyombo vya Habari, amesema wanachojua wao ni ushindi tu hivyo Mwadui watawasamehe kwa hilo.

”Mwadui tunawaheshimu sana walitufunga mechi ya kwanza na pia tuliwafunga kwa taabu sana kwenye hatua ya mtoano ya Kombe la shirikisho, lakini ni lazima wajue pointi tatu tunazihitaji hivyo tupo tayari kwa hilo”, amesema Manara.

Aidha Manara amesema mchezo utapigwa Saa 10:00 jioni kwenye uwanja wa taifa, tofauti na ambavyo imekuwa ikielezwa kuwa utapigwa Saa 11:00 jioni.

Simba inaongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 72 katika mechi 29, wakati Mwadui FC ina pointi 34 katika mechi 29 ikiwa katika nafasi ya 12 kwenye msimamo wa ligi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu