Juventus imekataa kumuuza winga Douglas Costa 28 licha ya Man United kuwa na hamu ya kumsajili baada ya mkufunzi Maurizio Sarri kuzuia uhamisho wa nchezaji huyo wa Brazil. (Mail)
Real Madrid itawasilisha ombi la kumsaini kiungo wa kati wa Tottenham Christian Eriksen msimu ujao iwapo Paul Pogba ataongeza kandarasi yake na Man United .
Eriksen mwenye umri wa miaka 27 atapatikana kwa uhamisho wa bila malipo kwa kuwa kandarasi yake inakamilika 2020. (Sky Sports)
Beki wa Real Madrid Sergio Ramos amemshauri Pogba, 26, kutoka Man United na kuhamia katika klabu hiyo ya Uhispania. (Express)
Chelsea imeanzisha mazungumzo na beki wa Itali Emerson, 25, kuhusu kandarasi mpya mpya. Winga wa England Callum Hudson Odoi 18 anakaribia kukamilisha mkataba mpya wa malipo ya £180, 000 kwa wiki katika mkataba wa miaka mitano.. (Express)
A