Sosopi aitaka NEC kusimamia uchaguzi kwa haki Monduli.

In Siasa

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA) Patrick Ole Sosopi ameitaka tume ya uchaguzi kusimamia uchaguzi wa jimbo la uchaguzi kuwa wa huru na haki katika jimbo la Monduli ili wananchi waweze kupata viongozi bora kupitia uchaguzi unazingatia sheria ,kanuni na misingi ya demokrasia.

Akizungumza na Wanahabari katika Ofisi za CHADEMA Wilayani hapo ambapo amesema kuwa iwapo sheria na kanuni zitaheshimiwa wataweza kuibuka na ushindi katika jimbo hilo kwani wana mgombea anayekubalika na wananchi.

Patrick amesema kuwa tayari wamejiandaa kufanya kampeni za kistaarabu katika vijiji vyote vilivyopo katika wilaya hiyo na kumnadi mgombea wao.

Mgombea wa kiti cha Ubunge kupitia chama hicho Yonas Laizer amesema kuwa baada ya uteuzi katika chama chake tayari wananchi wameonesha nia ya kumchagua hivyo anaamini ataibuka na ushindi katika uchaguzi huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu