Sudan yapokea mualiko kutoka Marekani.

In Kimataifa

Sudan imepokea mualiko kutoka Marekani wa mafunzo ya pamoja ya kijeshi na Misri, ukiwa ni mualiko wa kwanza wa aina hiyo kwa zaidi ya miongo mitatu.

Mkuu wa jeshi la Sudan, Jenerali Emad al-Din Adawi ametangaza mualiko huo wa mazoezi ya pamoja yajulikanayo kama Bright Star yatakayofanyika nchini Misri, baada ya kukutana na maafisa wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani wiki hii.

Mkuu huyo wa jeshi la Sudan amesema mkutano wao umefungua mlango kwa mazungumzo zaidi ambayo yanaweza kurejesha tena mahusiano kati ya Marekani na Sudan.

Mnamo mwezi Julai Marekani iliahirisha kwa miezi mitatu uamuzi wake wa kuiondolea vikwazo vya kiuchumi Sudan juu ya rekodi yake ya haki za binadamu na masuala mengine.

Uchumi wa Sudan umeporomoka tangu Sudan Kusini kujitenga mnamo mwaka 2011, na kuondoka na thuluthi tatu ya mafuta yanayozalishwa, chanzo chake kikuu cha fedha za kigeni na mapato ya serikali.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu