Sugu anyimwa dhamana arudishwa rumande.

In Kitaifa
Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini (CHADEMA) Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyassa, Emmanuel Masonga wamerudishwa rumande hadi Januari 22, 2018 siku ya Jumatatu ambapo kesi yake itaanza kusomwa mfululizo.
Mbunge huyo wa Mbeya mjini na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyassa wanashikiliwa na jeshi la polisi wakituhumiwa kutenda kosa la uchochezi katika mkutano wao wa hadhara ambao ulifanyika Disemba 31, 2017 jijini Mbeya ambapo jeshi la polisi linasema kuwa viongozi hao walizungumza maneno yenye kuleta chuki kati ya Serikali na wananchi.
Mchana wa January 16, 2018 Mahakama ya Hakimu Mkazi Jijini Mbeya iliamuru Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyassa Emmanuel Masonga wapelekwe rumande mpaka January 19 ambayo ni leo kwa kesi ya uchochezi.
Viongozi hao wamerudishwa rumande tena mpaka siku ya Jumatatu ambapo kesi yao itaanza kusomwa tena

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu