Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Mh Rashid Taka amepiga marufuku hotel zote kubwa za kitalii kuuza bidhaa za
kitamaduni kwani kuendelea kuuza bidhaa hizo ni kuwanyima fursa wenyeji kufanya biashara hizo za kitamaduni na hivyo kutoa miezi 4 mpaka kufikia tarehe 30 juni wawe wamemaliza kuuza bidhaa za kitamaduni zilizopo kwenye hoteli zao au kuzirudisha katika maboma ya kitamaduni (cultural tourism) .
Ametaka bidhaa hizo za kitamaduni ziwe zinauzwa katika maboma ya kitamaduni ili kulinda na kutunza utamaduni wa wenyeji badala ya kuwaibia ujuzi na ubunifu wao.
Ametoa katazo /agizo hilo wakati wa ugawaji wa mifugo 624 walipatikana kupitia boma la utalii wa kitamaduni la Ndemwa lililopo katika kata ya Olbalbal Wilaya ya Ngorongoro.