Taliban wamteua balozi wao kwenye UN

In Kimataifa

Taliban wameomba kuhutubia viongozi wa dunia kwenye mkutano wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York wiki hii.

Wamemteua msemaji wao alioko Doha Suhail Shaheen kama balozi wa Afghanistan kwenye Umoja huo, kulingana na barua ambayo shirika la habari la Reuters limeiona Jumanne.

Waziri wa mambo ya nje wa Taliban Amir Khan Muttaqi amewasilisha ombi hilo katika barua iliyotumwa kwa katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Antonio Guterres Jumatatu.

Muttaqi aliomba kuzungumza wakati wa kikao cha ngazi ya juu cha baraza kuu la Umoja wa mataifa ambacho kilimalizika Jumatatu.

Msemaji wa Guterres, Farhan Haq amethibitisha barua hiyo ya Muttaqi.

Haq anasema barua ya Taliban ya kutaka wapewe kiti kwenye Umoja wa mataifa ilitumwa kwa kamati ya nchi 9 wanachama, ikiwemo Marekani, China, na Russia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu