TANZANIA YAONDOLEWA KIKWAZO

In Kimataifa

Rais mpya wa Marekani Joe Biden amewaondolea raia wa Tanzania vikwazo vya kushiriki bahati nasibu ya viza, mwaka mmoja baada ya kutangazwa kwa vikwazo hivyo.

Januari 30, 2020 serikali ya Donald Trump ilitangaza kuwawekea Watanzania vikwazo vya kushiriki bahati nasibu hiyo pamoja na raia wa nchi nyingine kadhaa.

Kwa mujibu wa afisa mmoja mwandamizi wa utawala uliopita wa Trump, nchi hizo ziliwekewa marufuku hiyo kwa kushindwa kufikia kiwango stahiki cha ulinzi na kupashana taarifa.

“Nchi hizi, kwa sehemu kubwa, zinataka kutoa msaada lakini kwa sababu mbali mbali zimefeli kufikia viwango vya chini tulivyoviweka,” aliyekuwa Naibu Waziri wa Usalama wa Ndani wa Marekani Chad Wolf aliwaambia wanahabari baada ya kutangazwa kwa vikwazo.

Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania umetangaza kuwa marufuku hiyo imefutwa rasmi na rais mpya wa nchi hiyo Joe Biden aliyeingia madarakani juzi Jumatano.

“Mojawapo kati ya hatua zake za mwanzo kabisa akiwa Rais, Rais Biden ameondoa kikwazo kilichowekwa kwa Watanzania kuomba Viza ya Bahati Nasibu (Diversity VISA – DV),” ubalozi huo umeandika kupitia ukurasa wake wa Twitter

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu