Jeshi la Israel linasema limeanza kushambulia maeneo yanayodhibitiwa na jeshi la Iran nchini Syria.
Kikosi cha ulinzi Israel (IDF) kinasema operesheni yake ni dhidi ya kikosi cha Quds – kikosi maalum katika jeshi la mapinduzi la Iran.
Haikutoa ufafanuzi zaidi. Lakini kuna taarifa kuhusu makombora yaliofyetuliwa katika maeneo yanayo uzunguka mji mkuu wa Syria, Damascus mapema Jumatatu.
Vyombo vya habari nchini Syria vinasema vikosi vya ulinzi wa angani vimezuia ‘shambulio la Israel’. Siku ya Jumapili jeshi la Isarel lilisema limezuia kombora katika eneo la Golan Heights.