Juventus iko tayari kubadilishana wachezaji ambapo mpango huo utamfanya winga wa Juvetus Christiano Ronaldo kujiunga na PSG huku mshambuliaji wa Brazil Neymar akielekea Juventus. (Tuttomercato – in Italian)
Hatahivyo , Ronaldo anafikiria kurudi katika klabu yake ya zamani Manchester United.
Babake Lionel Messi ambaye pia ni ajenti wake amekana ripoti kwamba mshambuliaji huyo ana mipango ya kujiunga na PSG kutoka Barcelona msimu. (Goal)
Manchester United inapanga kumuuza kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba 27 wakati wa dirisha la uhamisho la msimu ujao.. (Talksport)