Klabu ya AC Milan inasaka saini ya winga wa Crystal Palace
Wilfried Zaha mwezi Januari na inaamini kwamba mchezaji hyo
mwenye umri wa miaka 28 wa Ivory Coast anaweza kuwasaidia
kupata taji la kwanza la Serie A katika kipindi cha miaka 10.
(Sun)
Milan pia ina matumaini ya kuafikiana mkataba wa kumzuia
kipa wa Itali mwenye umri wa miaka 21 Gianluigi Donnarumma
katika klabu hiyo. (Corriere Della Sera – in Italian)
Mshambuliaji wa Uhispania Diego Costa, 32, ameambia klabu
ya Atletico Madrid anataka kandarasi yake kufutwa na
kuondoka katika klabu hiyo katika dirisha la uhamisho la
mwezi. (Goal)
Arsenal inafikiria kufanya uhamisho wa ghafla wa
mshambulikaji huyo wa zamani wa Chelsea , huku Gunners
wakiwa na mpango wa kuongeza mshambuliaji mwengine. (AS
via Express)
Iwapo Costa atajiunga na wapinzani wao wakuu katika ligi ya
La liga Real Madrid, Barcelona au Sevilla, timu yake mpya
italazimika kulipa £22.7m. (El Mundo)