Trump ametangaza hali ya hatari kulinda mawasiliano ya nchi dhidi ya maadui.

In Kimataifa

Rais Donald Trump ametangaza hali ya dharura kwa ajili ya kuilinda mifumo ya kompyuta dhidi ya ” wapinzani wa kigeni”

Rais huyo wa Marekani amesaini sheria ya utaratibu wa utendaji ambayo inazuwia mara moja makampuni ya Marekani kutumia mawasiliano ya kigeni yanayoaminiwa kuhatarisha usalama wa nchi hiyo.

Bwana Trump hataji kampuni yoyote katika agizo hilo.

Hata hivyo, wachambuzi wanasema uamuzi huo unailenga kampuni kubwa ya mawasiliano ya Kichina Huawei.

Nchi kadhaa- Marekani ikiwemo-zimekwisha elezea wasi wasi wake kwamba huduma za kampuni hiyo zinaweza kutumiwa na Uchina kwa upelelezi. Huawei imesema kuwa kazi yake haisababishi tisho lolote.

Kwa mujibu wa msemaji wa Ikulu ya White House, agizo la Bwana Trump linalenga “kuilinda Marekani dhidi ya wapinzani wake ambao wamekuwa wakionekana kubuni mbinu za kutumia taarifa na mifumo ya teknolojia ya mawasiliano pamoja na huduma zake “.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu