Trump amevitembelea vikosi vya Marekani nchini Afghanistan.

In Kimataifa

Rais wa Marekani Donald Trump amevitembelea vikosi vya Marekani nchini Afghanistan ikiwa ni ziara ya kushtukiza na kusema kuwa Marekani na Taliban wamekuwa katika mazungumzo.

”Taliban iko tayari kukubaliana,” Trump aliviambia vikosi katika kambi ya jeshi la angaa la Bagram, ikiwa ni ziara yake ya kwanza nchini humo, ambapo pia alikutana na raisi wa nchi hiyo, Ashraf Ghani.

Ziara hiyo imekuja baada ya mpango wa kubadilishana mfungwa na mwanamgambo wa Taliban wakati wa kuanza kwa mazungumzo ya amani.

Bwana Trump amesema kuwa Marekani ilikuwa kwa kiasi kikubwa inapunguza idadi ya wanajeshi wake.

Wanajeshi 13,000 wa Marekani wanasalia nchini Afghanistan miaka 18 baada ya Marekani kuingilia kati kupambana na wanamgambo wa Taliban baada ya mashambulizi ya tarehe 11 mwezi Septemba mwaka 2001.

Ziara ya Trump inafanyika majuma kadhaa baada ya Taliban kuwaachia hutu wanazuoni wawili wa kutoka nchi za magharibi ambao walikuwa wakishikiliwa mateka tangu mwaka 2016, raia wa Marekani Kevin King na wa Australia Timothy Weeks wakibadilishwa na viongozi wa juu watatu wa wanamgambo hao.

”Tunakutana nao (Taliban) na tunasema lazima mapigano yakome na hawakutaka kukomesha mapigano na sasa wanataka kuweka silaha chini,” Trump alisema kwenye kambi hiyo iliyo karibu na mji mkuu, Kabul.” Ninaamini tutafanikiwa namna hiyo.”

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu