Trump amfukuza mkuu wa usalama wa mitandao aliyekanusha madai ya wizi wa kura

In Kimataifa

Rais Donald Trump wa Marekani amemfuta kazi mkurugenzi wa shirika la usalama na miundombinu ya mtandao, kwa kukosowa kauli yake juu ya wizi wa kura kwenye uchaguzi wa Novemba 3. Trump ametumia akaunti yake ya Twitter kumfukuza kazi Christopher Krebs, akisema kauli yake ya hivi karibuni kutetea usalama wa uchaguzi ilikuwa si sahihi hata kidogo. Kufukuzwa kwa Krebs kunakuja wakati Trump akiendelea kukataa kuyatambuwa matokeo ya uchaguzi huo ambao mpinzani wake mkuu kutoka chama cha Democrat, Joe Biden, alishinda. Krebs si afisa wa kwanza anayeshuku madai ya Trump kufutwa kazi. Mnamo tarehe 9 Novemba, alimfukuza kazi Waziri wa Ulinzi Mark Esper katika juhudi za kuweka watu wanaomtii kwenye nafasi za juu ya wizara hiyo. Krebs ndiye aliyekuwa akiliongoza shirika hilo la usalama wa mitandaoni tangu lilipoanzishwa mara tu baada ya uchaguzi wa 2016, ambao ulitajwa kuingiliwa na Urusi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu