Trump azungumzia hali katika mpaka wa Mexico na Marekani

In Kimataifa

Rais wa Marekani, Donald Trump amesema hali iliyopo katika mpaka wa Marekani na Mexico inazidi kuwa mbaya na imegeuka kuwa mzozo. Kauli hiyo ameitoa jana usiku katika Ikulu ya Marekani wakati akilihutubia taifa. Trump amesisitiza kuwa hatua ya kushindwa kuwadhibiti wahamiaji haramu, inawaumiza mamilioni ya wananchi wa Marekani. Amesema mzozo wa kibinaadamu na kiusalama unaongezeka katika mpaka huo uliopo kusini mwa Marekani. Rais Trump amesema kila siku maafisa wa forodha na walinzi wa mpakani wanakabiliana na maelfu ya wahamiaji haramu wanaojaribu kuingia nchini Marekani. Kiongozi huyo amerudia wito wake wa kujengwa ukuta katika mpaka huo, akisema ni muhimu kwa usalama kwenye mpaka huo. Spika wa Baraza la Wawakilishi, Nancy Pelosi amemuonya Trump aache kuishikilia serikali ya Marekani mateka kwa kutengeneza mzozo kwenye mpaka huo na amemtaka azifungue baadhi ya shughuli za serikali ambazo zimefungwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu