Tume ya Uchaguzi Congo yaairisha kuotoa Matokeo.

In Kimataifa
Tume ya uchaguzi ya DRCongo imechelewesha kutangaza matokeo ya awali ya uchaguzi wa rais,huku kukiwa ongezeko la mbinyo kutoka mataifa yenye nguvu na kanisa Katoliki kuheshimu matakwa ya wapiga kura.

Matokeo ya  awali, ambayo  yalipangwa kutolewa  leo Jumapili, sasa yatatolewa  wiki  ijayo, mkuu  wa  tume  ya  uchaguzi  nchini  humo CENI ameliambia  shirika  la  habari  la  AFP masaa  machache kabla  ya  muda  wa  mwisho  kumalizika.

“Haitawezekana  kutangaza  matokeo  siku  ya  Jumapili. Tunapinga hatua , lakini  hatuna  kila  kitu bado,” alisema Corneille Nangaa, bila ya  kutangaza  siku ya kutangaza  matokeo hayo.

Baraza  la maaskofu  wa  Kanisa  Katoliki  lenye ushawishi  mkubwa nchini  Congo , CENCO, ambalo  linawakilisha  maaskofu  wa Kikatoliki  nchini  humo , limeonya  kwamba  hasira za umma zinaweza  kujitokeza iwapo matokeo  ya  mwisho hayatakuwa  ya “kweli kwa mujibu wa matokeo halisi  ya  kura.”

Kanisa katoliki  lenye ushawishi nchini  Congo, ambalo limetoa  zaidi ya  wachunguzi  wa  uchaguzi  40,000 , lilisema  siku  ya  Alhamis kwamba  linamjua mshindi  wa  uchaguzi  huo , lakini  halikumtaja.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu