Tumekusogezea Ratiba nzima ya mazishi ya KING MAJUTO

In Kitaifa
Kufuatia  kifo cha msanii nguli wa vichekesho nchini, Mzee Amri Athumani aliyeaga dunia jana usiku majira ya saa 2:00 usiku katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa akitibiwa, mtoto wa marehemu ametoa ratiba ya kuaga na mazishi ya nguli huyo.
Mwili wa Marehemu Mzee Majuto utaswaliwa na kuagwa katika Msikiti ulipo ndani ya Hospitali ya Muhimbili wakati wa Swalat Dhuhr (Swala ya Mchana) leo Agosti 9, 2018 na baadaye utapelekwa katika Viwanja vya Karimjee vilivyopo Posta jijini humo kwa ajili ya waombolezaji wengine na mashabiki zake kupata fursa ya kumuaga.
Baada ya Swalat L’laasir (Swala ya Alasiri), majira ya saa 9 mchana mwili wa marehemu Mzee Majuto utasafirishwa kwenda nyumbani kwake Mkoani Tanga ambako maziko yatafanyika kesho Ijumaa baada ya Swalat Dhuhr ( Swala ya Mchana) Tanga Mjini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu