Tunashukuru kwa ahadi ya dola Bilioni 6 kwa Syria-O’Brien

In Kimataifa

Mkuu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa mataifa Stephen O’Brien amekaribisha ahadi ya wahisani ya takribani dola bilioni 6 ili kuisaidia Syria na ukanda mzima kwa mwaka 2017 ikiwa ni ahadi kutoka kwa wahisani 41.

Dola zingine bilioni 3.7 zimeahidiwa na wahisani haohao kwa ajili ya mwaka 2018 na zaidi.

Hata hivyo wakati zahma kubwa kabisa ya kibinadamu na wakimbizi Syria ikiingia mwaka was aba , mustakhbali wa watu na taifa hilo bado uko njia panda ameonya O’Brien.

Umoja wa mataifa na washirika wake waliohudhuria mkutano wa kimataifa wa usaidizi kwa ajili ya Syria mjini Brussels Ubelgiji wanalenga kuwafikia watu milioni 12.8 mwaka huu walio ndani ya Syria na nje kama wakimbizi.

O’Brien amesema mkutano huo kwa ajili ya Syria umemalizika na nia moja ya kimataifa, kuendelea kusaidia mgogoro huo na mamilioni ya watu wanaohitaji msaada.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu