Tuzo za Mo Simba Awards zaanzishwa.

In Michezo

Mwekezaji katika klabu ya Simba, Mohammed Dewji ameanzisha tuzo maalum ambazo amezipa jina la Mo Simba Awards na zitakuwa zikitolewa kwa wachezaji, viongozi na mashabiki wa klabu hiyo.

Tuzo hizo zitakazofanyika kwa mara ya kwanza tarehe 11 mwezi Juni katika Hoteli ya Hyatt Regency zinalenga kutambua mchango wa wachezaji, viongozi na mashabi ambao juhudi zao zimeiwezesha Simba SC kupata mafanikio iliyonayo sasa.

Utolewaji wa tuzo hizo utaleta changamoto kwa wachezaji kujituma zaidi kwani washindi wa tuzo zitakazotolewa katika vipengele mbalimbali watakuwa na deni kuhakikisha msimu ujao wanaendelea kufanya vizuri ili wabaki kwenye tuzo.

Kwa wachezaji ambao hawatapata tuzo ni wazi kwamba wataongeza bidii ili kufanya vizuri kuweza kushinda tuzo wakati mwingine jambo ambalo litaleta faida kwa klabu.

Vilabu kama Manchester United barani Ulaya vimekuwa na utamaduni wa kutoa tuzo mwishoni mwa msimu kwa wachezaji mbalimbali waliofanya vizuri hivyo mpango huu aliokuja nao Mo Dewji utakuwa na tija kwa klabu ya Simba.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu