Uchaguzi wa Palestina waahirishwa

In Kimataifa

Rais wa mamlaka ya ndani ya Palestina Mahmoud Abbas ametangaza jana kuwa uchaguzi wa Palestina uliopangwa kufanyika mnamo Mei 22 umeahirishwa kwa muda usiojulikana.

Abbas ametoa tangazo hilo baada ya mkutano na wawakilishi wa makundi kadhaa ya wapalestina mjini Ramallah na kusema uchaguzi huo hautafanyika hadi serikali yake itakapopata hakikisho kuwa eneo la Jerusalem Mashariki pia litashiriki kupiga kura.

Duru kutoka Palestina zinasema uamuzi huo unatokana na Israel kushindwa kuridhia matakwa ya mamlaka za Palestina za kuruhusu upigaji kura kufanyika pia kwenye eneo hilo la mji wa Jerusalem ambalo linakaliwa kwa mabavu. Kundi la Hamas ambalo linatawala ukanda wa Gaza ulio sehemu ya mamlaka ya ndani ya Palestina limesema halikubaliani na uamuzi wa kuahirishwa kwa uchaguzi huo ambao ungekuwa wa kwanza katika kipindi cha zaidi ya miaka 15.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu