Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kusitishwa kwa muda mapigano.

In Kimataifa

Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kusitishwa kwa muda mapigano ili kuruhusu kiasi ya raia 20,000 waliozingirwa kwenye mji wa Raqqa, nchini Syria, waweze kuondoka.

Umoja huo pia umevitaka vikosi vinavyoongozwa na Marekani kusitisha mashambulizi ya anga ambayo yamesababisha majeruhi.

Mshauri wa masuala ya kiutu wa Umoja wa Mataifa nchini Syria, Jan Egeland amewaambia waandishi habari mjini Geneva, Uswisi, kwamba boti katika Mto Euphrates hazipaswi kushambuliwa na kwamba watu wanaotoka kwenye boti hizo hawawezi kuhatarisha maisha yao kwa mashambulizi ya anga.

Aidha, mjumbe msaidizi wa Umoja wa Mataifa nchini Syria, Ramzy Ezzeldin, amesema umoja huo bado unatathmini matokeo ya mazungumzo yaliyofanyika wiki hii mjini Riyadh kati ya makundi matatu ya upinzani ya Syria ambayo yalishindwa kuungana.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu