Vijana sita wa timu ya Burundi ya ubunifu wa Maroboti watoweka.

In Kimataifa
Vijana sita wa timu ya Burundi ya ubunifu wa Maroboti wameripotiwa kutoweka baada ya kushiriki katika mashindano ya kimataifa nchini Marekani.
Polisi imesema wawili kati ya vijana hao waliripotiwa kuonekana wakivuka mpaka wa Marekani kuingia Canada na kuongeza kuwa hakuna “dalili zozote za kutokea uhalifu”.
Hata hivyo Shirika la Huduma za Mpakani nchini Canada, limesema haliwezi kuthibitisha wala kukanusha kuwa vijana hao wawili waliingia Canada.
Wavulana hao wanne na wasichana wawili walionekana mara ya mwisho siku ya Jumanne mchana wakati mashindano hayo ya maroboti yalipokamilika mjini Washington.
Burundi kwa muda mrefu imekumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe na machafuko, na kuongezeka kwa mapigano kumewalazimu watu  laki  nne ,kuyakimbia makazi yao tangu Aprili 2015, wakati Rais Pierre Nkurunziza aliposema atagombea muhula wa tatu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu