Wabunge wa Ufaransa waidhinisha mswaada kukabiliana na wimbi la nne la Covid-19

In Kimataifa

PARIS,Bunge la Ufaransa leo hii limeridhia muswada ambao utafanya chanjo ya Covid-19 kuwa ya lazima kwa wafanyakazi katika sekta ya afya pamoja na takwa la kuviongezea nguvu vithibitisho vya afya kwa maeneo ya kijamii ya wazi.Hatua hiyo inaridhiwa wakati Ufaransa ikikabiliana na wimbi la nne la maambukizi ya virusi vya corona. Tayari wanaohudhuria katika majumba ya makumbusho, sinema au mabwawa ya kuogelea wanazuiwa kuingia katika maeneo hayo kama hawataonesha vithibitisho vya kupata chanjo ya Covid-19 au kufanya vipimo vya karibuni kabisa dhidi ya virusi vya corona.Vithibitisho hivyo kwa kiwango kikubwa vinahitajika katika matamasha au katika vilabu vya starehe. Lakini kwa sasa kuanzia mwezi ujao wa Agosti, nyaraka hizo zitahitajika zaidi katika kuingia katika migahawa, baa, na pia kwa safari za muda mrefu za treni na ndege.Kama ilivyo kwa mataifa mengine ya Ulaya, Ufaransa ipo katika makabliano na kizazi kingine cha virusi vya corona aina ya Delta ambacho kinaambukiza kwa kwa kasi. Kirusi hicho ambacho kimegudulika kwa mara ya kwanza nchini India, kinatishia kuongeza muda zaidi wa makabiliano ya janga la corona na kufifisha jitihada za mataifa katika kufufua uchumi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu