Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema idadi ya wagonjwa wa corona imefikia 13 ambapo kati yao 8 ni Watanzania na watano ni wageni
Waziri Ummy ameyabainisha hayo leo Machi 26, 2020, wakati akitoa taarifa kwa umma, kuhusu hali ya maambukizi ya virusi vya Corona nchini
Amesema kati ya wagonjwa hao Dar es Salaam wapo nane, Arusha wawili, Zanzibar wawili na Kagera mmoja.