Wahamiaji 117 kutoka waliokuwa wamezuiliwa Libya wamewasili nchini Rwanda mapema leo asubuhi, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la wakimbizi UNHR.
Wengi wa wahamiaji wa kundi hili la sasa wanatoka katika nchi za Eritrea na Somalia.
Muungano wa Ulaya awali uliilipa mamilioni ya euro kwa nchi ya Niger ambayo inawahifadhi wakimbizi zaidi ya 4,000 ambao walikuwa wanashikiliwa nchini Libya ili kuwazuwia kuendelea kuingia Ulaya.
Maafisa wa Rwanda wamesema kuwa hawana makubaliano na Muungano wa Ulaya, wala hawana faida rasmi kutokana na kuwapokea wakimbizi.
Kundi hili linafuatia Kundi jingine la wahamiaji 66 lililojumuisha nalojumuisha watu watu walio hatarini zaidi pamoja na watoto walio peke yao ambalo liliwasili nchini humo wakiwemo watoto.