Wanawake wameshauriwa kuwa na mazoea ya uhudhuria kwenye semina mbalimbali za ujasiriamali ikiwa ni pamoja na kujishughulisha na biashara mbalimbali ili waweze kujikimu kimaisha na kutowategemea waume zao.
Wito huo umetolewa na mkurugenzi wa kampuni inayojihusisha na maswala ya wanawake sambamba na ujasiriamali wa kuku ijulikanayo kama ARIANA POULTRY INVESTMENT Tumaini Mkadimba, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na umuhimu wa mwanamke kujituma ambapo amesema mwanamkw anapaswa kusimama imara katika familia ili kuweza kuinua kipato
Tumaini amesema kuwa wamekuwa wakiandaa makongamano mbalimbali ya kuhamasisha wanawake kuwa wajasiriamali ambapo wametafanya kwa takribani miaka mitano ambapo lengo ni kumtoa mwanamke kuroka hatua moja kwenye nyingine
Amesema kuwa ushiriki wa mwanamke katika mapinduzi ya viwanda ni muhimu sana kwani ukimwelimisha mwanamke mmoja umeelimisha jamii hivyo akawataks wanawake kuwa na uthubutu wa kuanzisha biashara
Amesema hivi karibuni ameandaa kongamano maalumu la wanawake ushiriki wa mwanamke katika tanzania ya viwanda ikiwa ni pamoja na kuwafundisha umiliki wa biashara, utaftaji wa masoko, namna ya utunzaji wa fedha na uwekezaji, ambapo atawaunganisha na wadau mbalimbali
Hata hivyo kongamano hilo litafanyika katika ukumbi wa Corido spring ambapi amewataka wanawake kutumia fursa hiyo ili waweze kufikia malengo yao.