Wapiganaji 35 wauawa katika mapigano na jeshi DRC.

In Kitaifa

Na:Semio Sonyo (News Room)/RFI

Jeshi la Serikali ya DRC limesema kuwa jumla ya wapiganaji wa waasi 35 kutoka kundi la Mai Mai linaloongozwa na William Yakutumba wameuawa katika operesheni Sokola ya pili mjini Fizi, huku jeshi hilo likipoteza askari wake 15 na wengine 19 kujeruhiwa.
Jeshi la Congo linasema limefanikiwa kuwakamata wapiganaji kadhaa pamoja na silaha za kijeshi zilizokuwa zinatumiwa na wapiganaji hao.

Jenerali anayeongoza operesheni hiyo, Jenerali Yav Philemon amesema jumla ya wapiganaji 70 wamekamatwa na wengi walijisalimisha wenyewe na kuthibitisha kujeruhiwa kwa kamanda wa waasi hao Yakutumba na kumkamata naibu wake Ekanda Byamungu.

Jenerali Philemon akayaonya makundi mengi ya waasi ambayo yameendelea kutatiza usalama kwenye eneo la mashariki mwa nchi hiyo.

Operesheni ya jeshi la Congo tayari imesababisha maelfu ya raia kukimbia maeneo yao.

Wengi walikimbilia nchi jirani za Burundi na Tanzania.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu