Wapinzani CONGO waungana

In Kimataifa
Vyama viwili vikuu vya upinzani vya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo vimeungana baada ya kujiondoa kwenye muungano wa awali uliomuweka mgombea mmoja kushindana na yule anayeungwa mkono na Rais Joseph Kabila.

Kwa mujibu wa makubaliano yaliyotangazwa siku ya Ijumaa (23 Novemba) mjini Nairobi, Kenya, sasa Felix Tshisekedi anayeongoza chama kikubwa zaidi cha upinzani cha UPDS atasimama kwa niaba ya chama chake na kile cha spika wa zamani, Vital Kamerhe.

Uamuzi huu umefikiwa ikiwa ni mwezi mmoja tu kabla ya uchaguzi wa tarehe 23 Disemba kwenye taifa hilo tajiri kwa madini la Afrika ya Kati.

Tangazo hili linamaanisha kwamba uchaguzi huu utakuwa na pande tatu kuu zinazowania: Emmanuel Ramazani Shadary anayeungwa mkono na Kabila, Martin Fayulu anayeungwa mkono na viongozi wawili wakuu wa upinzani waliozuiwa kuwania urais – Jean-Pierre Bemba na Moise Katumbi, na Tshisekedi anayeungwa mkono na Kamerhe.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu