Washambuliaji wauwa wakristo sita kanisani Burkina Faso.

In Kimataifa

Watu wenye bunduki wamelivamia kanisa la kikatoliki katika mji wa Dablo nchini Burkina Faso na kuuwa watu sita jana Jumapili. Kulingana na duru za maafisa wa serikali, waumini walikuwa wakishiriki katika ibda ya asubuhi, wakati walipozingirwa na kundi la wavamizi takriban ishirini walioanza kuwafyatulia risasi. Washambuliaji hao walilichoma kanisa, kisha wakalitia moto duka moja na magari mawili. Mwezi Aprili, wakristo wengine 5 waliuawa katika shambulizi lililolenga kanisa la kiprotestanti katika mji mdogo wa Silgadji pia nchini Burkina Faso, mchungaji akiwa miongoni mwa wahanga. Miji ya Dablo na Silgadji iko Kaskazini mwa Burkina Faso, eneo ambalo limekuwa likiandamwa na mfululizo wa mashambulizi ya umwagaji damu, ambayo inaaminika yanafanywa na makundi ya kigeni yenye itikadi kali, yakiwemo Ansarul Islam, Kundi la Kulinda Waislamu na Uislamu-GSIM, na Dola la Kiislamu katika eneo la Sahara.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu