Washiriki 16 wasusia shindano la Miss Burundi 2018

In Burudani
Warembo 16, waliokuwa wanashiriki shindano la kumtafuta Miss Burundi wamejiondoa katika hatua ya fainali iliyopangwa kufanyika Julai 21, 2018 na kupelekea shindano hilo kuhairishwa mpaka Julai 28, mwaka huu.
Hali iliyopelekea nchi ya Burundi kuingiwa na hofu kubwa ya kupatikana kwa mlimbwende atakaye iwakalisha nchi hiyo kimataifa kwa mwaka 2018 katika mashindano yenye mlengo wa kuonyesha utamaduni, uweledi na urembo wa mwanamke wa Burundi.
Hata hivyo warembo hao wamefikia maamuzi hayo ya kususia shindano hilo kufuatia madai kuwa shindano la mwaka huu kumefanyika udanganyifu mkubwa upande wa zawadi itakayozawadiwa kwa mshindi wa kwanza na mshindi wa pili.
Ambapo waandaaji wa shindano hilo, Burundi Event hapo awali walitangaza washindi hao kujinyakulia gari, kiwanja chenye mita mraba 400 pamoja na hundi ya pesa taslimum, cha kushangaza ni kwamba walimbwende hao wanadai kuwa hakuna maandalizi yeyote ya zawadi hizo.
Aidha kufuatia mzozo huo wanakamati watano wa shindano hilo waliamua kuchukua uamuzi wa kujiudhulu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu