Watanzania watakiwa kucheki afya zao na kufuata ushauri wa daktari.

In Afya

Watanzania wametakiwa kuwa na mazoea ya kwenda vituo vya afya kucheki afya zao na kuacha dhana ya kutumia dawa bila kufuata ushauri wa daktari
Wito huo umetolewa na Dr,Meshak Athman mkurugenzi wa Yeriko Sanitarium Clinic wakati akizungumzia namna watu wanavyoshindwa kutofautisha magonjwa ambapo amesema ugonjwa unaokuwa ni changamoto ni UTI na KISONONO ambayo ni magonjwa ya zinaa


Amesema kisonono dalili zake ni wakati wa kushiriki tendo la ndoa kwa mwanaume inaonesha dalili kwa haraka hasa kwenye mfumo wa haja ndogo, ndani ta masaa 12 hadi 24 na kupata maumivu makali wakati anapoenda haja ndogo na usaha mzito,
Pia amesema dalili za UTI ni kupata haja ndogo mara kwa mara, kupata maumivu ya tumbo la chini, kutoka uchafu mweupe kwenye haja ndogo 


Dr. Meshak amesema kuwa ni vizuri watu kufanya vipimo ili kuweza kujua ugonjwa unaokusumbua kwani watu wengi wamekuwa wakitumia dawa nyingi sana ambazo hazisaidii kumaliza tatizo na badala yake kuleta madhara makubwa ambayo tanaweza kupelekea hata kupoteza maisha
Pia amewataka watanzania kuchukua taadhari kabla ya kupata madhara kwenye miili yao ikiwa ni pamoja na kuacha ngono zembe, kula vyakula vyenye virutubisho na kufanya mazoezi mara kwa mara

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu