Watu 30 wafariki dunia DRC baada ya boti kuzama.

In Kimataifa

Watu wasiopungua 30 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 200 hawajulikani walipo baada ya boti kuzama kwenye ziwa huko magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Meya wa mji wa Inongo Simon Mboo Wemba, amelieleza shirika la habari la AFP kuwa boti hiyo ilikuwa imebeba abiria zaidi ya 350, na kwamba watu waliookolewa ni 182 pekee. Ajali hiyo ilitokea usiku wa Jumamosi katika ziwa Mai-Ndombe. Wemba ameongeza kwamba imekuwa vigumu kuhesabu idadi kamili ya abiria kwasababu wengi wanahofiwa kuwa wahamiaji haramu. Usafiri wa mito na maziwa ni moja ya usafiri unaotumiwa sana nchini Congo. Mwezi uliopita kiasi ya watu 167 walifariki katika ajali mbili tofauti za majini na kumfanya rais Felix Tshisekedi kutoa amri ya kila abiria kufaa jaketi la uokozi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu