Watu wawili wameuwawa na wengine wanne wamejeruhiwa vibaya huko Venezuela.

In Kimataifa
Watu wawili wameuwawa na wengine wanne wamejeruhiwa vibaya hapo jana katika ghasia za nchini Venezuela wakati upinzani wa kisiasa ulipoitisha kura ya maoni isiyo rasmi ya kupinga mipango ya Rais Nikolas Maduro ya kuiandika tena katiba ya nchi.
Kulingana na msemaji mkuu wa upinzani, watu wenye silaha waliokuwa wamepanda pikipiki walikishambulia kituo cha kupigia kura katika mji wa Catia, kaskazini magharibi mwa mji mkuu wa Caracas.
Taifa hilo lenye utajiri wa mafuta linakabiliwa na mgogoro mbaya wa kiuchumi kuwahi kutokea, huku kukiwa na uhaba wa mahitaji kadhaa ya msingi pamoja na mfumko wa bei wa hali ya juu.
Zaidi ya watu 90 wameuwawa katika maandamano ya kila siku ya kuipinga serikali iliyopo madarakani yaliyoanza tokea mwezi Aprili mwaka huu.
Maduro ambaye amekataa kuachia madaraka, pia ameitisha kura ya maoni baadaye mwezi huu ya kuteua kamati maalumu itakayoandika upya katiba ya taifa hilo la Amerika Kusini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu