Watu zaidi 50 wauawa kwa shambulio la Boko Haram.

In Kimataifa

Idadi ya vifo inayotokana na shambulio la kundi la Boko Haram dhidi ya timu ya utafutaji wa mafuta kaskazini mashariki mwa Nigeria mapema wiki hii imeongezeka hadi kufika watu zaidi ya 50.

Likinukuu vyazo vya kijeshi, kitabibu na makundi ya kutoa misaada ya kiutu, shirika la habari la Kifaransa la AFP limesema idadi ya vifo ni kubwa kuliko ile iliyotolewa na maafisa wa serikali, na kwamba maiti bado zinaendele kuwasili katika kitio cha afya.

Shambulio hilo la Jumatano iliyopita lililenga timu ya Shirika la Petroli la Kitaifa la Nigeria na wanajiolojia waliokuwa katika eneo la Ziwa Chad. Hapo jana, jeshi la Nijeria limesema kwamba watu watano kutoka katika kundi hilo wameuwawa, pamoja na wanajeshi kadhaa.

Eneo la kaskazini mashariki mwa Nigeria kwa miaka minane sasa limekuwa likishambuliwa na uasi wa kundi la misiamamo mikali ya kidini la Boko Haram,ambalo limesababisha vifo vya watu 20,000 na wengine milioni 2.7 kuyahama makaazi yao.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu