Thomas Thabane ametangaza kuwa atajiuzulu kama waziri mkuu wa Lesotho kufuatia miezi kadhaa ya shinikizo baada ya kutajwa kama mshukiwa katika mauaji ya aliyekuwa mkewe.
Hakusema ataachia madaraka lini lakini chama chake kimesema kuwa waziri mkuu mpya ataapishwa Jumatano.
Mke wa Thabane wa sasa (mke mdogo), ambaye alikuwa akiishi naye wakati aliyekuwa mkewe anauawa, alishtakiwa mwezi Februari kwa kuhusishwa na mauaji hayo.
Thabane mwenye miaka 80, na mkewe mdogo wamekanusha kuhusiaka na mauaji ya mke mkubwa.