Waziri Mkuu Majaliwa atembelea kiwanda cha sukari TPC kilichopo Arusha chini.

In Kitaifa

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea kiwanda cha sukari cha TPC kilichopo Arusha Chini, wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro na kukagua baadhi ya miundombinu ya kiwanda pamoja na mashamba.

Akiwa kiwandani hapo, Waziri Mkuu ameelezwa kwamba hivi sasa msimu wa uzalishaji umefungwa, na kiwanda kinafanyiwa matengenezo ambapo alishuhudia baadhi ya mitambo ikiwa imefunguliwa na kufanyiwa ukarabati.

Akitoa taarifa juu ya matengenezo hayo, Meneja wa Kiwanda hicho, Bw. Pascal Petiot , amemweleza Waziri Mkuu kwamba kiwanda hicho kimefungwa kwa zaidi ya wiki sita ili kujiandaa na msimu ujao wa uzalishaji ambao uko karibuni kuanza.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa kiwanda hicho, Bw. Robert Baissac amesema uzalishaji wa sukari kwenye kiwanda hicho umepanda kwa asilimia zaidi ya 200, tangu wachukue kiwanda hicho mwaka 2000.

Amesema wakati wanaanza, kiwanda kilikuwa na uwezo wa kuzalisha tani elfu 36,000 kwa mwaka, na wakati wanakinunua walitakiwa kuongeza uzalishaji kwa asilimia 100, kwa kufikisha tani 72,000 za sukari.

Aidha Waziri Mkuu aliwataka wafanyakazi wa kiwanda hicho, wafanye kazi kwa bidii na kujituma na kuhakikisha wanaongeza tija katika uzalishaji wao.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu