Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amewaacha mawaziri wake waandamizi katika nafasi zao wakati ameunda serikali mpya ya walio wachache akiungwa mkono na chama kidogo cha Ireland Kaskazini.

In Kimataifa
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amewaacha mawaziri wake waandamizi katika nafasi zao wakati ameunda serikali mpya ya walio wachache akiungwa mkono na chama kidogo cha Ireland Kaskazini.
Chama cha May cha Conservative kilipoteza wingi wa viti bungeni katika uchaguzi wa kitaifa uliofanyika siku ya Alhamis ambao chama cha upinzani cha Labour kilinyakua zaidi ya viti vipya 30.
May sasa ataongoza serikali pamoja na chama cha siasa za mrengo wa kulia cha Democratic Unionist – DUP, ambacho viti vyake 10 vitampa wingi wa viti kwa ajili ya kuongoza.
Waziri huyo Mkuu aliitisha uchaguzi wa mapema katika jaribio la kuiimarisha nafasi yake katika Umoja wa Ulaya wakati Uingereza ikijiandaa kujiondoa katika Umoja huo.
Badala yake, Mbunge wa Labour David Lemmy anahisi kuwa uchaguzi huo umedhoofisha mamlaka yake.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu