Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amesema uchumi wa nchi ukitengemaa, serikali itaongeza posho za madiwani na watendaji wa vijiji.

In Kitaifa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amesema uchumi wa nchi ukitengemaa, serikali itaongeza posho za madiwani na watendaji wa vijiji.

Simbachawene amesema hayo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema).

Nassari alikuwa ametaka kusikia serikali itaongeza lini posho ya watendaji hao ambapo Simbachawene amesema, Serikali inatambua mchango wa viongozi hao katika maendeleo ya nchi, lakini kutokana na uchumi kutotengemaa, haiwezi kuwaongeza posho.

Akijibu swali la Mbunge wa Musoma Mjini, Vedasto Manyinyi (CCM), Naibu Waziri wa Nchi, ofisi ya Rais (Tamesemi), Seleman Jafo alisema serikali inatambua mchango wao katika kusimamia shughuli za maendeleo. Katika swali lake la msingi, Manyinyi alitaka kujua kama serikali imeridhika na malipo ya wenyeviti wa mitaa na madiwani hao.

Jafo amesema majukumu yanayotekelezwa na viongozi hao ni utekelezaji wa dhana na ugatuaji wa madaraka, kwa wananchi ambapo mipango yote uamuzi unafanyika katika ngazi za msingi wa serikali za mtaa.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu