Wito watolewa na Waziri wa Mambo ya nje wa China kuziondoa silaha za kinyuklia katika rasi ya korea.

In Kimataifa

Waziri wa mambo ya nje wa China ametoa wito wa kuondoa silaha za kinyuklia katika rasi ya Korea, huku mvutano juu ya mipango ya makombora na silaha za kinyuklia ya Korea Kaskazini ukiwa unazidi kupamba moto.

Wang Yi amewaambia maripota wa mjini Athens baada ya kukutana na mwenzake wa Ugiriki, Nikos Kotzias, kwamba China inaunga mkono kikamilifu kuondolewa kwa silaha zozote za kinyuklia katika eneo hilo, ili kupatikane utulivu na amani.

Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka China kuchukua hatua imara, kuishinikiza Korea Kaskazini kusitisha mipango yake ya kinyuklia na makombora ya masafa marefu.

Katika wiki za hivi karibuni, Korea Kaskazini imekuwa ikitishia kujibu mashambulizi yoyote ya uchokozi.

Aidha shirika la habari la Yonhap la taifa hilo, limeripoti leo hii kwamba raia mmoja wa Kimarekani amekamatwa akiwa anajaribu kuikimbia Korea Kaskazini.

Ni raia wa tatu wa Kimarekani kushikiliwa nchini humo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu