ZAIDI YA MILIONI 200 ZIMETOLEWA KWA AJILI YA KUREKEBISHA MIUNDOMBINU YA BARABARA KATIKA KATA YA MURIETI JIJINI ARUSHA DIWANI WA KATA YA MURIETI FRANSIS MBISE AMEZUNGUMZA NA VYOMBO VYA HABARI NA KUELEZEA HALI HALISI
Akizungumza na vyombo vya habari Diwani wa kata ya Muriet jijini Arusha Mh. Frances Mbise amesema kuwa, kata ya Murieti ni kata ambayo ina mkusanyiko mkubwa wa watu kuliko kata zote na mvua zilizonyesha ziliharibu sehemu mbalimbali jambo linalopelekea wananchi kushindwa kufanya shughuli zao
Amesema kutokana na hayo basi serikali imeanza kuifanyia marekebisho baaddhi ya maeneo kama barabara ya Bon site, Kwa patel, Nabosoito, na sehemu mbalimbali ambapo wamekuwa kipaombe kushirikiana na serikali ili kuweza kuleta maendeleo
Amesema kuwa utekelezaji huo umeshaanza ambapo marekebisho ya barabara bado yanaendea na kuna baadhi ya maeneo wameweka vifusi ili kuweza kupisha wananchi kuendelea na majukumi
“Tunaishukutu serikali ya awamu ya tano kwa kuwajali wananchi wake kwani wametoa fedha hizo kwa ajili ya mapenzi ya kweli na wananchi wake na changamoto kubwa ni ujenzi kusitishwa kutokana na mvua zinazoendea kunyesha na kusitisha ujenzi lakini ujenzi huo utakamilika mvua zikipungua” amesema Mh Mbise
Pia amechukua fursa hiyo kutoa wito kwa wananchi kutokana na janga la corona kujitahidi kuzingatia kanuni na elimu zinazotolewa na wadau wa afya namna ya kujikinga ikiwa ni pamoja na kuepukana na misongamano isiyo ya ulazima