Zambia: Jeshi la polisi limemtia mbaroni kiongozi wa chama kidogo cha upinzani.

In Kimataifa

Jeshi la polisi nchini Zambia hapo jana limemtia mbaroni kiongozi wa chama kidogo cha upinzani nchini humo cha United Progressive Party ambaye ni mkosoaji wa Rais Edgar Lungu.

Kukamatwa kwa mwanasiasa huyo ni hatua ya hivi karibuni dhidi ya wapinzani wa kisiasa nchini Zambia.

Savior Chishimba ambaye ni kiongozi wa chama cha United Progressive Party alikamatwa na maafisa wa polisi baada ya kuonekana katika mahojiano kwenye kituo kimoja cha televisheni ya binafsi mjini Lusaka.

Rais wa Zambia Edgar Lungu mwezi uliopita alitangaza kuchukua hatua zaidi za kiusalama ambazo zinalipa mamlaka zaidi jeshi la polisi kuwatia mbaroni watu huku pia kiongozi huyo akivishutumu vyama vya upinzani nchini humo kwa kuhusika na vitendo vya vurugu.

Hakainde Hichilema kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Zambia cha United Party for National Development amekuwa gerezani tangu mwezi April.

Rais Egar Lungu amekuwa akikanusha madai kuwa anajaribu kuunda utawala wa kiimla na anawashutumu mahasimu wake kisiasa kwa kutaka kubadilisha matokeo ya uchaguzi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu