Zimbabwe itajenga chuo kwa gharama ya dola bilioni moja

In Kimataifa

Zimbabwe itajenga chuo kwa gharama ya dola bilioni moja, kwa hemisha ya mtu anayelaumiwa kwa kuiongoza nchi kuelekea hali ngumu ya uchumi, Robert Mugabe.

Jonathan Moyo, ambaye ni waziri wa elimu aliwaambia waandishi wa habari kuwa wanachukua hatua hiyo kwa heshima ya rais huyo wa umri wa miaka 93, kwa wajibu wake katika elimu na uongozi mzuri.

Haijulikani pesa hizo zitatoka wapi kwenye nchi ambayo ukosefu wa ajira na umaskini ni tatizo kubwa.

Mwaka uliopita zaidi ya watu watu milioni moja nchini Zimbabwe walikumbwa na ukosefu wa chakula kotokana na ukame. Nchi hiyo wakati mmoja ilitajwa kuwa ghala la Afrika.

Licha ya hilo baraza la mawaziri limekubali kutumia dola milioni 800 kujenga chuo hicho kipya huko Mazowe, kilomita 35 nje ya mji wa Harare.

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu