Zomeazomea yasababisha COSATU kukatisha hotuba ya Rais Zuma katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi nchini Afrika Kusini

In Kimataifa

 Muungano wa vyama vya wafanyakzi nchini Afrika Kusini Cosatu umelazimika kukatisha ghafla hotuba za kuadhimisha siku ya wafanyakazi ikiwemo hotuba iliyokuwa ikitarajiwa kutolewa na Rais Jacob Zuma baada ya umati kuanza vurugu na baadhi yao kumzomea Zuma.

Rais huyo na ujumbe wake walionekana wakiondoka haraka kutoka kwenye jukwaa la maadhimisho hayo na kuchukuliwa na msafara mkubwa wa magari.

Cosatu ambao ni mshirika muhimu kisiasa wa chama tawala cha Afrika Kusini African National Congress ANC mwezi uliopita ulimtaka Zuma kujiuzulu baada ya kumuachisha kazi waziri wa fedha na kusababisha kushushwa kwa uwezo nchi hiyo kukopesheka.

Misururu ya maandamano imefanyika nchini humo kwa miezi kadhaa sasa kumshinikiza Zuma kuachia madaraka kutokana na kashfa za ufisadi na uongozi mbovu.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu