In Kitaifa

Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa imewasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya mwaka 2017/2018, huku ikisisitiza kuwa hali ya ulinzi na usalama wa mipaka ya nchi kwa ujumla ni shwari licha ya kuwepo kwa changamoto katika baadhi ya nchi ,za ukanda wa Afrika Mashariki maziwa makuu na pembe ya Afrika.

Akiwasilisha bajeti jana  bungeni mjini Dodoma waziri wa wizara hiyo dokta HUSSEIN MWINYI, ametaja maeneo hayo kuwa ni pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Burundi, Somalia na Sudan Kusini.

Amesema uwepo wa hali ya matishio ya ugaidi wa kimataifa ulivilazimu vyombo vya ulinzi na usalama kwa kushirikiana,na nchi jirani na raia wake kuendelea kuwa katika hali ya tahadhari na umakini ili endapo kutajitokeza dalili yoyote inayotishia usalama, hatua stahiki ziweze kuchukuliwa haraka.

Akizungumzia vitendo vya uhalifu dokta MWINYI amesema katika kukabiliana na vitendo hivyo wizara kupitia Jeshi la Wananchi la Tanzania(JWTZ), imeendelea kushirikiana na vyombo vingine vya usalama na mataifa mengine katika kupambana na matishio ya kiusalama yakiwemo ugaidi, uharamia na biashara haramu ya dawa za kulevya.

Naye mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ADADI RAJABU ameishauri serikali kulipatia fedha za maendeleo zilizoidhinishwa na Bunge fungu 38, Ngome ambalo linahusika na mambo ya msingi kwa uwepo wa nchi na kwa kuwa kasma za matumizi muhimu zipo katika fungu hilo.

 

Wizara hiyo imeomba kiasi cha shilingi  trilioni 1.725 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na matumizi ya maendeleo ili iweze kutekeleza majukumu yake.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu