Afisa wa afya wa Yemen amesema zaidi ya watu 96,000 wameambukizwa maradhi ya kipindupindu katika mlipuko uliosababisha vifo vya watu wapatao 746 tokea mwezi Aprili.

In Kimataifa

Afisa wa afya wa Yemen amesema zaidi ya watu 96,000 wameambukizwa maradhi ya kipindupindu katika mlipuko uliosababisha vifo vya watu wapatao 746 tokea mwezi Aprili.

Nasser al-Argaly, katibu wa afya katika serikali inayoongozwa na uasi mjini Sanaa, amesema mlipuko huo wa kipindupindu umetokana na kampeni ya mashambulizi ya miaka miwili inayongozwa na Saudi Arabia dhidi ya waasi wa jamii ya Houthi.

Mapigano hayo yameharibu miundombinu na kusababisha kuwepo uhaba wa dawa.

Maafisa wa afya nchini Yemeni wamesema ndege zilizokuwa zimebeba misaada ya kiutu ya tani 50 za dawa za maradhi ya kipindupindu kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu, ziliwasili katika mji wa kusini wa Aden, ambao unadhibitiwa na vikosi vya serikali.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu