Afisa wa afya wa Yemen amesema zaidi ya watu 96,000 wameambukizwa maradhi ya kipindupindu katika mlipuko uliosababisha vifo vya watu wapatao 746 tokea mwezi Aprili.

In Kimataifa

Afisa wa afya wa Yemen amesema zaidi ya watu 96,000 wameambukizwa maradhi ya kipindupindu katika mlipuko uliosababisha vifo vya watu wapatao 746 tokea mwezi Aprili.

Nasser al-Argaly, katibu wa afya katika serikali inayoongozwa na uasi mjini Sanaa, amesema mlipuko huo wa kipindupindu umetokana na kampeni ya mashambulizi ya miaka miwili inayongozwa na Saudi Arabia dhidi ya waasi wa jamii ya Houthi.

Mapigano hayo yameharibu miundombinu na kusababisha kuwepo uhaba wa dawa.

Maafisa wa afya nchini Yemeni wamesema ndege zilizokuwa zimebeba misaada ya kiutu ya tani 50 za dawa za maradhi ya kipindupindu kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu, ziliwasili katika mji wa kusini wa Aden, ambao unadhibitiwa na vikosi vya serikali.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu