Afisa wa serikali ya Kenya amesema wafanyakazi 4 wa misaada nchini Kenya, wamepoteza maisha baada ya gari yao kukanyaga bomu karibu na kambi ya wakimbizi ya Dadaab, katika kaunti iliyoko mashariki mwa Garissa.

In Kimataifa

Afisa wa serikali ya Kenya amesema wafanyakazi 4 wa misaada nchini Kenya, wamepoteza maisha baada ya gari yao kukanyaga bomu karibu na kambi ya wakimbizi ya Dadaab, katika kaunti iliyoko mashariki mwa Garissa.

 

Mohamud Saleh mratibu wa mkoa wa kaskazini mashariki, amesema gari hilo ni mali ya shirika la African Development Solutions.

Amesema inadhaniwa kuwa bomu hilo lilikuwa limetegeshwa na kikundi cha siasa kali ya Al-Shabab, ambacho kiko nchi ya jirani ya Somalia.

Inaelezwa kuwa zauidi ya watu 34 wamepoteza maisha mpaka sasa wakiwemo maafisa wa polisi 20, katika milipuko nchini humo katika kipindi cha wiki tatu zilizopita.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu